Psalms 7:1-5

Sala Ya Mtu Anayedhulumiwa

Ombolezo la Daudi kwa Bwana kwa sababu ya Kushi, Mbenyamini.

1 aEe Bwana, Mungu wangu, ninakukimbilia wewe,
uniokoe na kunikomboa na wote wanaonifuatia,
2 bla sivyo watanirarua kama simba
na kunichana vipande vipande, asiwepo wa kuniokoa.

3 cEe Bwana, Mungu wangu, kama nimetenda haya
na kuna hatia mikononi mwangu,
4 dau ikiwa nimemtenda uovu aliye na amani nami,
au nimemnyangʼanya adui yangu pasipo sababu,
5 ebasi adui anifuatie na kunipata,
auponde uhai wangu ardhini
na kunilaza mavumbini.
Copyright information for SwhNEN